Balozi wa Tanzania nchini China, Dkt. Suleiman Haji Suleiman, ameeleza kuwa makampuni kutoka nchini China yamevutiwa na uwezo mkubwa na kazi nzuri zilizofanywa na wanafunzi wa mkondo wa Amali.
Hayo
aliyasema Agosti 18, 2026 wakati wa ufunguzi
wa Maonesho ya Kitaifa ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayoendelea Viwanja
vya Shule ya Sekondari yaa Usagara Jijini Tanga ambapo Waziri wa Elimu ,
Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolph Mkenda alikuwa mgeni rasmi.
Balozi
Suleiman Haji Suleiman alisema kutokana
na umahiri huo, makampuni hayo yako tayari kutoa ufadhili wa masomo na mafunzo
kwa wanafunzi hao hapa Tanzania na nchini China, pamoja na kuwapa ajira ya moja
kwa moja baada ya masomo.
Katika hatua nyingine Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa. Carolina Nombo amesema Tanzania imejipanga kuishangaza dunia katika mashindano ya ujuzi kwa vijana baada ya kuanza kuwaandaa kwa kiwango cha kimataifa washindi wa nafasi za juu.
Prof. Nombo
amefafanua kuwa Tanzania sasa ni mwanachama wa Shirika la Mashindano ya Ujuzi
Duniani - WorldSkills Competition, hivyo imeanza kushiriki mashindano ya
kimataifa kufuatia maelekezo ya viongozi wa ngazi za juu.
"Kwa hiyo Tanzania tumeanza na tutahakikisha tunawaandaa vijana wetu kuonesha ujuzi wao wa kiwango cha juu ili dunia nayo itambue kuwa tuna vijana mahiri ambao wanaweza kushindana kwenye majukwaa ya kimataifa," amesema.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa. Carolina Nombo akizungumza.








0 Comments