.......................
Na Dotto
Mwaibale
SERIKALI ya
Mapinduzi (SMZ), Tume ya Taifa ya UNESCO pamoja na Taasisi ya Sanze Connect
kuandaa kongamano la Kimataifa la Utamaduni.
Lengo la
kongamano hilo ambalo litafanyika kuanzia Mei 16 hadi 21, 2026 limelenga
kuitangaza Zanzibar kama kitovu cha urithi na diplomasia ya utamaduni duniani.
Naibu Katibu
Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Khamis Abdalla Said akiongoza kikao cha kuratibu maandalizi ya
Kongamano hilo alisema ni la muhimu sana.
“Kongamano hilo la Kimataifa la Utamaduni (International Cultural Summit) ni la muhimu sana nan i hatua inayolenga kuitangaza Zanzibar kama kitovu cha urithi na diplomasia ya utamaduni duniani,” alisema Said.
Katika kikao
hicho kilichofanyika Aprili 15, 2026
katika ofisi za wizara, kilihusisha wadau wa kimataifa na kitaifa wakiwemo Tume
ya Taifa ya UNESCO na Taasisi ya Sanze Connect, pamoja na watendaji wa idara
mbalimbali za wizara hiyo.
Ili kuhakikisha
ufanisi wa maandalizi hayo, kikao kiliangazia maeneo kadhaa muhimu :
Ushirikiano
wa Kimataifa: Kuimarisha mahusiano kati ya Zanzibar na jumuiya ya kimataifa
kupitia nyanja za sanaa, utamaduni, na michezo kama nyenzo ya kukuza uchumi wa
buluu na utalii.
Maingiliano
ya Kitaasisi: Kujenga mfumo thabiti wa mawasiliano kati ya Tume ya UNESCO na
SANZE Connect katika kufanikisha malengo ya Summit hiyo.
Usimamizi wa
Idara: Kuhakikisha idara zote za wizara zinafanya kazi kwa ushirikiano ili
kuleta taswira chanya ya nchi wakati wa kongamano hilo.
"Kikao
hiki ni dira katika kuhakikisha Zanzibar inatumia fursa ya International
Cultural Summit kuonesha utajiri wake wa kiutamaduni na vipaji vya vijana wetu
katika jukwaa la kimataifa," alieleza Naibu Katibu Mkuu wakati wa kikao
hicho.
Kikao hicho
kilihitimisha hatua ya kwanza ya upangaji mikakati, kikisisitiza dhamira ya
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuendeleza sekta za ubunifu na michezo
kama nguzo muhimu za maendeleo ya kijamii










0 Comments