MWASISI WA KIGODA CHA CCM MTANDAONI AMPONGEZA RAIS SAMIA KUTUNUKIWA TUZO YA UDAKTARI

MWASISI WA KIGODA CHA CCM MTANDAONI AMPONGEZA RAIS SAMIA KUTUNUKIWA TUZO YA UDAKTARI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

...........................

Na Dotto Mwaibale, Dodoma

 Mwasisi wa Kigoda cha Chama Cha Mapinduzi (CCM), Taifa Mtandaoni, Balozi wa Amani Tanzania na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Kata ya Iganjo Jimbo la Uyole Jijini Mbeya, Suma Oddo Lwena  amempongeza  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayoifanya  na kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (PhD), kutoka Chuo Kikuu cha Jimbo la Nasarawa cha nchini Nigeria.

 Shahada hiyo ya heshima alitunukiwa Aprili 11, 2026 kwa njia ya mtandao.

“ Kazi nzuri anayoifanya Rais wetu ndiyo sababu ya kutunukiwa tuzo hiyo kwetu sisi kama nchi nimafanikio makubwa,” alisema Lwena.

Lwena aliongeza kuwa Shahada hiyo ya Heshima aliyotunukiwa ni kutokana na kuchagiza matumizi ya  nishati safi ya kupikia, afya ya mama na mtoto, taswira nzuri katika masuala ya uongozi kwa wanawake Afrika na jinsi anavyosimamia masuala ya biashara hususani kwa vijana wa Afrika.

Mwasisi wa Kigoda cha Chama Cha Mapinduzi (CCM), Taifa Mtandaoni, Suma Addo Lwena.
 

Post a Comment

0 Comments