Katibu wa Hasama wa Seneti ya Vyuo Vikuu na Vyuo Mkoa wa Dodoma, Ajoki Mwakatebe akizungumza wakati wa Kambi Maalumu ya Mafunzo inayoendelea mkoani humo ambayo itafikia tamati Aprili 9, 2026.
...............................
KAMBI ya Seneti ya Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dodoma imekuwa na mafanikio kufuatia washiriki kujitokeza kwa wingi licha ya wanafunzi wengi kuwa kwenye likizo.
Katibu wa Hasama wa Seneti hiyo Mkoa wa Dodoma, Ajoki
Mwakatebe akizungumzia kambi hiyo alisema ni kwa ajili ya mafunzo maalumu ya siku tatu ambayo imewahusisha
washiriki zaidi ya 440 wa mkoa huo.
“Kambi hii ya siku
tatu ilianza Aprili 7, 2026 na itafikia tamati kesho Aprili 9, 2026 imekuwa na
mafanikio makubwa kutokana na maudhurio mazuri ya washiriki zaidi ya 440 kutoka
wilaya zote za Mkoa wa Dodoma na isingekuwa wanafunzi kuwa likizo idadi
ingekuwa kubwa zaidi ,” alisema Mwakatebe.
Mwakatebe alisema katika mafunzo hayo mada zilizotolewa
zilihusu wajibu na majukumu ya vijana kwa CCM, Ujenzi wa hoja na matumizi ya
mitandao na siasa za mitandao.
Alitaja maada nyingine kuwa ni dhana ya ujamaa katikaa siasa
na uchumi wa kisiasa, dhana ya kazi za
chama, mahusiano kati ya chama na Serikali, itikadi na imani ya CCM na dhana ya
ulinzi wa chama.
Aidha, Mwakatebe alitaja mada zingine kuwa ni maandalizi ya
uchaguzi wa chama na jumuiya na Itifaki ya chama na jumuiya.
Alisema siku ya kwanza ya mafunzo hayo walianza na mdahalo
ambao ulihusu nafasi ya kijana katika kuleta matokeo chanya ndani ya CCM na
maendeleo ya Tanzania kwa ujumla.
Washiriki wakiwa kwenye kambi hiyo.
Katibu wa UVCCM Wilaya ya Kibaha Mjini, Joel Kituu, akichangia jambo kwenye mafunzo hayo.
Washiriki wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea.
Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale simu namba 0755362990













0 Comments