SEGEREA YA ITIKA BONNAH AKICHUKUA FOMU YA UBUNGE

SEGEREA YA ITIKA BONNAH AKICHUKUA FOMU YA UBUNGE

 Msimamizi wa Uchaguzi   wa INEC katika  majimbo ya Segerea, Kivule, Ukonga na Ilala, Faraja Nakua. akimkabidhi fomu Mgombea Ubunge Jimbo la Segerea Bonna Kamoli jijini Dar es Salaam Agosti 26, 2025.

......................................

MAELFU ya wanachama, wapenzi  wa Chama Cha Mapinduzi  (CCM) na wananchi  katika Jimbo la Segerea, wilayani Ilala, jijini Dar es Salaam,   wamejitokeza kumsindikiza Mgombea Ubunge wa  jimbo hilo  Bonna Kamoli, kuchukua  fomu  ya  uteuzi katika Ofisi za  Tume  Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC)  wilayani humo.

Msafara mrefu wa magari, pikipiki na  bajaji wa mgombea huyo  uliopambwa kwa shamrashamra, ngoma, matarumbeta  na nyimbo za  kuisifu  CCM   ulianzia  katika eneo la Tabata Shule, majira ya saa 6:00 mchana, kupitia Tabata   Segerea, kisha kuingia Barabara ya Segerea-Majumba Sita na kuingia Barabara ya Nyerere kisha  Mtaa wa Lumumba  zilipo ofisi ndogo za INEC.  

Bonnah, alipanda gari linalofunguka kwa juu na  kujitokeza katika paa la gari hilo  huku akipunga mkono na kupeperusha  bendera  ya CCM katika mitaa msafara huo ulipopita.

Mgombea huyo alikabidhiwa fomu na  Msimamizi wa Uchaguzi   wa INEC katika  majimbo ya Segerea, Kivule, Ukonga na Ilala, Faraja Nakua.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa fomu hizo, Bonnah aliwaomba wananchi wa Segerea kumpa kura nyingi na za kishindo mgombea urais    kwa tiketi ya CCM,  Dk. Samia Suluhu Hassan  na yeye mwenyewe.

Bonna Kamoli akionesha begi lenye fomu baada ya kukabidhiwa.Maandamano na shamrashamra za uchukuaji wa fomu zikiendelea.Taswira ya maandamano ya tukio zima la uchukuaji


 

Post a Comment

0 Comments