KATIBU MKUU CCM DKT. ASHA-ROSE MIGIRO KUPOKELEWA RASMI LEO DODOMA

KATIBU MKUU CCM DKT. ASHA-ROSE MIGIRO KUPOKELEWA RASMI LEO DODOMA

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Balozi Dkt. Asha Rose Migiro
..............................

Na Dotto Mwaibale

WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wananchi leo wanatarajiwa kujitokeza kwa wingi kumpokea Katibu Mkuu wa Chama  hicho Dkt. Asha- Rose Migiro atapowasili katika Ofisi za Makao Makuu ya  CCM jijini Dodoma.

Dkt. Migiro anatarajiwa kuwasili katika ofisi hizo kuanzia saa 2:00 asubuhi.

Kikao cha Halmashuri Kuu ya CCM (Taifa) chini ya Mwenyekiti wake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kilichoketi Agosti 23, 2025 kilimteua Dkt. Migiro (Balozi) kushika nafasi ya katibu mkuu wa chama hicho.

Wananchi na wana CCM wanakaribishwa kushiriki katika tukio hilo la kihistoria ambapo Dkt. Migiro anakuwa mwanamke wa kwanza kuwa Katibu Mkuu wa CCM Taifa.

Post a Comment

0 Comments