Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinzuzi (UVCCM), chini ya Mwenyekiti wake Mohamed Ali Kawaida Mei 24, 2025 wamezindua Kampeni Maalum ya Kijani First time voters Mkoani Dodoma ambapo maelfu ya vijana wamejitokeza kushiriki katika tukio hilo la kihistoria lililobeba agenda ya kuwahimiza vijana watakaopata sifa ya kupiga kura kwa mara ya kwanza kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2025,
Kijani First Time voters ni muendelezo wa Kampeni mama ya “Tunazima zote Tunawasha kijani” Iliyoanzishwa kwa malengo ya kuhamasisha makundi mbalimbali ya watanzania katika kushiriki uchaguzi na kuchagua wagombea wa CCM kuanzia ngazi ya Madiwani na Ubunge na Mgombea Urais Dkt.Samia Suluhu Hassan.









0 Comments