MBUNGE WA CHALINZE RIDHIWANI KIKWETE ASHIRIKI MAPOKEZI YA ALLY HAPI BAGAMOYO

MBUNGE WA CHALINZE RIDHIWANI KIKWETE ASHIRIKI MAPOKEZI YA ALLY HAPI BAGAMOYO

Mbunge wa Chalinze ambaye pia ni  Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Mhe.Ridhiwani Kikwete, akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa (MNEC), Ally Hapi wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani.


.........................................


Na Mwandishi Wetu, Bagamoyo.


Mbunge wa Chalinze ambaye pia ni  Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Mhe.Ridhiwani Kikwete, ameshiriki mapokezi ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa (MNEC), Ally Hapi na mkutano wa hadhara wakati wa ziara ya MNEC huyo wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

Pamoja na kupokea ugeni huo ametumia nafasi hiyo kuwaeleza wananchi mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya 2020/ 2025.

Aidha, Kikwete amewakumbusha wananchi kujiandikisha katika daftari la ukaazi na kupiga kura na kuwahimiza kuendelea kuamini kuwa serikali ya CCM chini ya Uongozi wa Rais Samia Suluhu Hasan bado inaendelea kutekeleza majukumu yake vizuri.

"Wana Bagamoyo tuna kila sababu ya kuendelea kumuunga mkono Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa aliyotufanyia ya kutuletea maendeleo," alisema Kikwete.   

Mbunge wa Chalinze ambaye pia ni  Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Mhe.Ridhiwani Kikwete, akiteta jambo na MNEC Ally Hapi wakati wa ziara hiyo.

Mbunge wa Chalinze akihutubia kwenye mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
 

Post a Comment

0 Comments