Mbunge wa Jimbo la Hanang Mhe Asia Halamga akiishiriki hafla fupi ya Mama lishe ya kuvunja mzunguko wa Mwaka 2025 iliyofanyika Desemba 30, 2025.
......................................
Na Dotto Mwaibale
KIONGOZI bora ni yule anayewajali wananchi wake na
kushirikiana nao katika shughuli za maendeleo, furaha na huzuni pasipo
kuwabagua jambo ambalo linawafanya wawe pamoja kuanzia ngazi ya shina hadi
Taifa.
Mbunge wa Jimbo la Hanang Mhe Asia Halamga ni mmoja wa
viongozi bora ambaye anaonesha njia kwa kuwajali wananchi wake katika masuala
ya maendeleo, furaha na huzuni amekuwa nao bega kwa bega liwake jua inyeshe
mvua yeye na wananchi wake.
Licha ya kuwa na umri mdogo kwa muda mfupi tangu awe
kiongozi akiwa mbunge kupitia kundi la vijana na sasa mbunge wa jimbo tumeona
mambo mengi aliyoyafanya na Mungu anavyoendelea kumpa kibali cha kuwatumikia
wananchi kwa nidhamu na unyenyekevu mkubwa na siyo kwa kuigiza.
Tumemuona ambavyo amekuwa akishirikiana nao katika matukio
ya huzuni kama misiba, shughuli za maendeleo na furaha ambapo Desemba 30, 2025
alishiriki hafla fupi ya Mama lishe ya kuvunja mzunguko wa Mwaka 2025 ambapo
alichangia jumla ya Sh. Milioni 2 kwa ajili ya kuwaunga mkono ili waweze kuimarisha
shughuli zao za kiuchumi.
Jambo hilo siyo dogo kwani wahenga wanasema ukiwainua
wanawake kiuchumi unakuwa umeliinua Taifa kutokana na umuhimu wao katika jamii.
Halamga jicho lake la maendeleo linaona mbali kwani anaunga
mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu
ambaye anamatamanio ya kuona kila mtanzania anainuka kiuchumi kwa msaada wa
viongozi mbalimbali kama Halamga ambao wanaonesha kuwiwa kuwatumikia wananchi
kwa dhati na vitendo na siyo blabla.
Wanawake hao walitumia nafasi hiyo kumshukuru mbunge wao kwa
msaada huo na kumtakia afya njema na heri yam waka mpya wa 2026
Wakati huo huo jana Desemba 31, 2025 Mbunge Halamga,
alisherehekea ukaribisho wa mwaka mpya wa 2026 pamoja na watoto kutoka maeneo
mbalimbali ya Kata ya Bassotu ambapo alikula nao chakula pamoja na kuwapatia
vifaa vya shule madaftari na kalamu kwa ajili ya masomo yatakayo anza shule zitakapofunguliwa
mwezi huu wa Januari.
Diwani wa Kata ya
Bassotu, Rose Kamili, alimshukuru mbunge huyo kwa msaada wake alioutoa kwa
watoto hao.
Wanawake wakionesha mshikamano kwenye hafla hiyo.
Wanawake hao wakimzawadia zawadi mbunge wao Asia Halamga.
Mbunge wa Hanang' Mhe. Asia Halamga, akiwagawia juisi watoto wa Kata ya Basoutu katika hafla aliyoiandaa ya kukaribisha mwaka mpya wa 2026.
Mbunge wa Hanang' Mhe. Asia Halamga, akiwa katika picha ya pamoja na watoto wa kata hiyo.
Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale namba ya simu 0754362990.












0 Comments