Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Manyara, Yustina Arcadus Rahhi, akitoa zawadi kwa wagonjwa alipotembea Hospitali ya Wilaya ya Mbulu na Kituo cha Afya cha Dongobesh Januari 1, 2026. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Mhe. Michael Semundu na kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini Dkt. Emmanuel Nuwas.
....................................... 

Na Dotto Mwaibale

UONGOZI ni mamlaka au karama  ya kuwaonyesha watu njia kwa vitendo.

Kipimo cha uongozi ni jinsi gani kiongozi husika anaweza kuleta ushawishi kwa watu na kufikia maendeleo yaliyotarajiwa.

Kiongozi bora hana muda wa kulalamika bali anatafuta ufumbuzi wa matatizo ya wananchi au watu walio chini yake anao waongoza.

Yustina Arcadus Rahhi Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Manyara ni kiongozi bora ambaye anafanya kazi yake kwa kushirikiana na wananchi wote pasipo kuwabagua iwe katika furaha, huzuni na shughuli za maendeleo na hawatengi bali anakuwa nao sambamba akijua kuwa  ni jukumu lake kufanya hivyo.

Kutokana na uongozi wake bora uliotukuka Januari 1, 2025 aliwiwa kutembelea Hospital ya Wilaya ya Mbulu kwenda kuwajulia hali wagonjwa na kuwapa zawadi mbalimbali ikiwa ni kuwatakia kheri ya mwaka mpya wa 2026.

Jambo hilo siyo dogo linaonesha jinsi ya kiongozi bora anavyoshirikiana na wananchi wake ambao anawaongoza.

Mbunge Rahhi kwa kuwa ni kiongozi anaye shirikiana na wananchi na viongozi wenzake mkoani humo katika ziara hiyo aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Michael Semundu na Mbunge wa Mbulu Vijijini Dkt. Emmanuel Nuwas ambapo pia walitembelea Kituo cha Afya Dongobesh na kuwapa faraja kubwa wagonjwa kwa kuzungumza nao na kuwapatia zawadi.

Kwa nyakati tofauti viongozi hao wakizungumza na wagonjwa hao waliwasisitizia kuendelea kuiamini Serikali yao ambayo inaongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye amekuwa akifanya kazi kubwa ya kuwaletea maendeleo.

Aidha, viongozi hao walimpongeza na kumshukuru Mhe. Rais kwa namna ambavyo anawathamini wananchi na watumishi wa Wilaya ya Mbulu nan chi nzima kwa ujumla ambapo walitumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi kumuombea.

Baadhi ya wagonjwa na jamaa zao walimshukuru mbunge huyo, mkuu wa wilaya hiyo na Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini Dkt. Emmanuel Nuwas kwa ukarimu waliowaonesha wa kwenda kuwajulia hali pamoja na kuwapa zawadi kwa ajili ya kuukaribisha mwaka mpya wa 2026 na kumuelezea kuwa mbunge huyo kuwa anaacha alama ya kuwatumikia.

Mbunge Rahhi ni mama mpole, mwenye huruma na mpenda maendeleo na mchapa kazi ambapo tangu ashike nafasi hiyo amekuwa na mchango mkubwa katika Mkoa wa Manyara na michango yake bungeni imekuwa ikionekana na kuleta tija.

Mmoja wa madaktari wa Hosptali hiyo akitoa maelezo kwa mbunge huyo na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu wakati wa ziara ya kutembelea hospitali hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Michael Semundu akizungumza na wagonjwa.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Manyara, Yustina Arcadus Rahhi, akitoa zawadi kwa wagonjwa.
Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini Dkt. Emmanuel Nuwas akimsalimia mgonjwa wakati wa ziara hiyo. Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Mhe. Michael Semundu.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Manyara, Yustina Arcadus Rahhi (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Michael Semundu (wa pili kushoto) na Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini Dkt. Emmanuel Nuwas (kulia) na viongozi wengine wakiwa na zawadi za ndoo na mabeseni walizozitoa kwa wagonjwa.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Manyara, Yustina Arcadus Rahhi, akisisitiza jambo wakati wa ziara hiyo.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Manyara, Yustina Arcadus Rahhi, akimjulia hali mgonjwa.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Manyara, Yustina Arcadus Rahhi, akiwapa juisi wagonjwa.

Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale namba ya simu 0754362990